HATUFIKI KWA SABABU TUNATUMIA NGUVU NA MUDA MWINGI KUJIULIZA "KAMA TUTAFIKA" BADALA YA KUANZA KWENDA Na Frazier Light





Kuna umuhimu wa kufika pointi ya kuelewa kwamba; Hakunaga miujiza kwenye swala zima la MAENDELEO na MABADILIKO. Kama ambavyo usipokula huwezi kwenda haja, vile vile USIPOWEKEZA huwezi KUENDELEA ama KUBADILIKA.

Mimi ni mpenzi sana wa soka, nikiwa na washkaji zangu juzi  tukiangalia mechi kati ya German vs Czech rafiki yangu mmoja akanifahamisha kitu ambacho kilinipa kutafakari. Kwa wale mnafuatilia soka mtakubaliana na mimi kwamba Ujerumani inaongoza kwa ubora wa soka duniani kwa sasa. Na ubora wao ni wa Takribani miaka 10 sasa! Na hata mpira wao ukitazama unaona kabisa hawa watu hawajaanza leo kucheza pamoja; wanacheza kama siafu.

Je! Wafahamu ya Kuwa Asilimia 90 ya kikosi chao kiliwekewa (Naiita Software) Kichwani kwao ya kuwa na “Mission” ya kuleta Kombe la Dunia Ujerumani tangu miaka zaidi ya 15 iliyopita? (Na walifanikiwa mwaka 2014 kule Brazil huku mwenyeji Brazil akipigwa goli 7). Mario Gotze, Draxler, Reus, Muller, Boateng; Wote walikuzwa chini ya “mradi” huu kwenye academy moja. Nuer, Ozil, Podolski, Khedira nao hivyo hivyo. 


Na sheria yao ujerumani ni kwamba huwezi kuwa kocha wa Taifa kama hujawahi kufundisha timu za watoto za Ujerumani (Academies under special projects). (kwa kuwa ndipo wanaposukia MISSION zao; Huku kwa wakubwa ni kumalizia tu)

Sasa Pata picha tangu mtoto yuko na miaka 5-10 na kuendelea; anachoambiwa ni kwamba kazi yako ni kuleta kombe la dunia kwenye taifa lako! Unafkiri watakuwa wa kawaida!? Cheza yao haiwezi kuwa ya kawaida. Kwa Nchi nyingi za Ulaya kila timu ina academy; na karibu kila shindano kubwa lazima litanguliwe na “juniors” Under 15,17…. Tofauti sana na huku Afrika, amabako tumeweka maslah mbele kwa kuteketeza “FUTURE” Hatuna pesa za kuendesha UMITASHUMTA ila tunazo za kushiriki Michuano ya Kombe la Dunia!!! Hahaha… Ni kituko sana hiki… Ni kama kumlazimisha tembo kupanda kwenye mti

Tutazame Tanzania kwa mfano; Kipindi kile Serengeti Boys ilipoanza, kizazi cha akina Nizar Khalfan, Mrisho Ngassa; Wakaja kuwa wachezaji wa kutegemewa kwenye timu ya Taifa! Tulijaribu vizuri. Ni vile tu tunahitaji “A WELL DEFINED PURPOSE AND LEADERSHIP”. Nguvu inayowekwa kwa Timu ya Taifa ya sasa, Nasikitika kusema tunamaliza pesa na matumaini bure. Tuwaige Uganda! Walikuwaga wabovu kuliko sisi, wakatulia chini, wakaanza kuwekeza kwa watoto, Wana wachezaji amabao wengine bado ni wanafunzi wa vyuo vikuu na High School, kwa sasbabu ni product waliyotoka nayo tangu udogoni. Leo hii wanamkaba koo Ghana, wanasumbua sana CECAFA na Kombe la mataifa Afrika.

HEBU JAMANI TUJIFUNZE. HAKUNA NJIA ZAIDI YA HII! LABDA TUNUNUE WACHEZAJI WA ACADEMY ZA ULAYA KISHA TUWAPE URAIA.

Ni wito wetu kwa Familia, Jamii, na Serikali; INAWEZEKANA. Ila itatuchukua muda na kweli tunahitaji muda. Tusikimbilie kupaua ilihali hatujaweka msingi wala kufunga lenta! Academy italeta tumaini la soka Afrika na Tanzania. Soka Lina Pesa SANA; Hebu tuamini kuwa kipaji kinatosha. KAMA MTOTO ANA KIPAJI NA SHULE HAIWEZI, USIMPOTEZEE MUDA. MPELEKE ACADEMY. KAMA HAKUNA ACADEMY AU HUWEZI KUGHARAMIA BASI WEKENI UTARATIBU NA M/KITI WA KIJIJI NA DIWANI WA KUWAPA MIPIRA NA UWANJA HAWA WATOTO, MTAANI HUKU TUNA MAKOCHA WAZURI TU. INAWEZEKANA WALA HAIHITAJI UFADHILI WA WATU WA MAREKANI.

Wakati niko Shule ya msingi, Nilikua nacheza mpira sana! Ila Nakumbuka watoto wenzangu ambao walikua wakicheza unavutiwa sana kuwatazama, unaona kabisa huyu mtu ni wa kipekee! Mnasema hakuna kama Messi na Ronaldo! Hujatembea vijijini na shule za changanyikeni uone watoto ambao wanapiga soka kama wamezaliwa na mpira. Unaona vitu ambavyo licha ya udogo walio nao, hata kwa Messi na Ronaldo huvioni. WAALIMU JAMANI; MU-ORGANIZE HAWA WENYE VIPAJI HUKO MASHULENI! MWANAFUNZI ANAWEZA ASIWE NA UWEZO DARASANI using’ang’anize ma REMIDUAL! Humsaidii… Ukifanya hivyo you will be concentrating on her weakest point! AND WE DON’T BUILD FROM WEAKNESS; WE BUILD FROM STRENGTH! Lazima kuna kitu yuko vizuri. HICHO HICHO KITUMIE KUBORESHA FUTURE ALIYO NAYO! Kazi ya mwalimu sit u kumsaidie mwanafunzi afaulu masomo ya darasani; ILA KUMSAIDIA MWANAFUNZI AJUE FUTURE ALIYONAYO NA VILE INAVYOWEZEKANA (Naandika hapa mpaka natamani walimu wotw duniani mungeelewa moyo wangu unachojaribu ku-communicate) Ualimu imekua kazi Fulani boring, wengine wanasema isiyokuwa na maslah, wengine wanasema ya kudharaulika kwa walimu wa kizazi hiki! Ila ni kwa sababu tu, hatujaweeza kuwaza nje ya chaki na kiboko! (Naamini kwenye makala nyingine tutazungumza zaidi juu ya hili)

Nihitimishe kwa kusema;

Sisi sote ni viongozi wa swala hili la Michezo… TUKIWEKEZA INAWEZEKANA. Mtoto asizeeke na KIPAJI chake.
  
Share on Google Plus

About The Light

0 comments:

Post a Comment