KIRUSI CHA UTUMWA ULIOKUMBA BARA LA AFRIKA KWA ZAIDI YA MIAKA 600; BADO NI GONJWA LA WAAFRIKA; Makala ya Frazier






Katika historia tumejifunza vile ambavyo kwa miaka zaidi ya 600, tulikua chini ya Ukoloni na utumwa. Willie Lynch katika barua yake ya mwaka 1712, kuhusiana na namna alivyokusanya watumwa alisema “Risasi tatu zinazotumika kumfanya mtu mtumwa ni: 1. HOFU, 2. KUUA IMANI (Ile hali ya kumpotezea mtu kujiamini) na 3. WIVU.

UTUMWA ni kirusi ambacho chenyewe hushambulia sana namna ya kufikiri ya jamii athirika. Na kisipotibiwa HUSAMBAA NA KUENDELEA KIZAZI HADI KIZAZI; hata kama minyororo imeshafunguliwa. Hakuna ugonjwa mbaya kama Utumwa wa fikra! Ni afadhali ule wa mijeledi na risasi.

Tazama mambo yafuatayo kisha utaelewa dhamira yangu:

Kama umesoma shule za msingi kama nilizosoma mimi, si jambo geni kuona mwalimu anakuja na mzigo wa fimbo darasani. Unaweza kukumbuka hofu unayojawa nayo kama mwanafunzi? Marafiki zangu kadhaa waliacha shule! (Kwenye hili; Unadhani akili ya mwanafunzi ingeweza kuelewa anachofundishwa?) (sasa ufikiri tu; kidogo, Je! kazi ya mwalimu ni kuchunga ng’ombe ama kumfanya mwanafunzi awe katika ubora ambao hata mwanafunzi mwenyewe haamini kama anaweza kuwa katika ubora huo?) Nidhamu ya saikolojia inasema “HOFU INAUA KUJIAMINI, NA KUTOKUJIAMINI KUNAUA UWEZO” (Na hakuna mwalimu ambaye hajasoma saikolojia, japo sio ile ya ndani sana ila ile ya kumpa mwanga) (Ila shida iko wapi hapa!) Tuhame hapa (Waweza Kutoa maoni yako kwenye sehemu ya “Comments”)

Wanafunzi wengi wa vyuo, haswa wanawake wanakumbana sana na kutakwa rushwa ya ngono ili wasaidiwe kufaulu (Mtakumbuka kile kisa cha mkufunzi aliyeshtakiwa wa chuo kimoja hivi majuzi). Hali Fulani ya mtu kutumia nafasi aliyonayo; kwa kua anafahamu una uhitaji na rungu kashika yeye, basi anatumia nafasi yake kukukandamiza. Tusikae sana hapa; yako mengi ya kutazama:

Juzi askari wa kutuliza ghasia (FFU) walitumia nguvu kubwa mno kumtia chini ya ulinzi mwanafunzi wa sekondari. Kilikua kitendo ambacho jamii yote ya watanzania ilikilaani. Haijalishi alifanya kosa gani ila njia iliyotumika haikua sahihi hata kidogo; hawawezi wakakosa namna nyingine kiasi kile cha kutumia nguvu ya namna ile. Tuhame pia hapa kwa muda

Tuje kwenye sehemu za kazi; pale unapoenda kwenye ofisi Fulani ukihitaji huduma Fulani; vile unavyosikilizwa kwa kuharakishwa na wakati mwingine dharau, wakati mwingine majibu yasiyo na kufikiri; mara kwa mara toa kitu kidogo! Hii hulka na akili matope ipo kwenye ofisi nyingi sana.

Tuje sasa kwenye kuyaconnect haya matukio na mada yangu. Binafsi naamini “Kama kazi yako haifanyi maisha ya watu kuwa bora; wewe ni tatizo kubwa sana kwenye huu ulimwengu! Na shida zipo kwa sababu wewe upo”

Najua hata kama hujawahi kwenda nchi za magharibi basi hata movie umewahi tazama! Vile askari anavyofanya kazi yake, lugha anayotumia, mtuhumiwa anavyoelezwa na kusikilizwa! Inadhihirisha kwamba huyu mtu anafanya hii kazi si kwa sababu alifeli darasani akakosa kazi nyingine. Huku kwetu unaona kabisa, huyu mtu hata hii kazi ni basi tu, kuna uwezekano hii haikua kazi ya ndoto yake! 

Kwa waliowahi kuvuka boda za Nchi moja ya Afrika kwenda nchi nyingine ya afrika wanaelewa ongea na samba la afisa na askari wa boda. Ila fika boda ya kwenda nchi za wenzetu; hadi raha yani, hata kama kuna kitu umekosea ama hujatimiza unasaidiwa kwa moyo wote. Mpaka unajiuliza hivi kwa nini waafrika tunachukiana hivi. Kwa nini hatupendi mwenzetu afanikiwe? Afurahi? Tuna shida gani kwenye akili zetu?

Kwa wale mliowahi kukumbana na ofisi za usajili wa mambo kadha wa kadha; kama ardhi, kampuni, shirika n.k! Moja kati ya jambo huwa najiuliza sana ni wasajili kazi yao ni nini? Si Kusajili? Mbona kama wanavyohusika na mahitaji ya wananchi ni kama vile kazi yao si kusajili ila kuzuia usajili! Maana utawekewa kila kikwazo na kila ugumu usio wa lazima. Ni kama kuna nati imefumuka kichwani ya wao kukumbushwa kuwa kazi yao ni kinyume cha wanachofanya. kama msajili unatakiwa uhuzunike na kuumia sana na kujiona umefeli pale mwananchi anaposhindwa kusajili swala lake! Kazi ya msajili ni kuhakikisha mambo hayashindikaniki kusajiliwa. Huduma yao ni kuhakikisha wanamsaidia mwananchi kusajili swala lake (na kama hajakidhi vigezo vilivyo nje ya uwezo wake, basi asaidiwe kukidhi vigezo hivyo)

Utumwa unatuua Waafrika; Mnaonaje wote tukaanza kufanya kazi zetu katika center ya kuhudumia watanzania na waafrika wenzetu nao wajione kuwa watu na waone hawaishi na wajerumani ama wakoloni wa kiingereza. Kwa nini usiipe kazi yako heshima kwa kutoa huduma kama professional? Unadharaulika sana kwa kuwa mtumwa wa fikra.

Wewe kama mkufunzi target yako yapaswa kuwa wanafunzi wako wawe bora kwenye ufaulu na ufanisi wa kazi. 

Wewe kwa nafasi yoyote uliyonayo yapaswa uishi kwa lengo la kazi yako kuleta amani, furaha na utoshelevu kwa wanajamii wako!

Huko kwenu kuna watumwa? Watu ambao wanatumia kazi zao kujiona wako juu sana kuliko wewe! Hawa ndio watumwa. Mtu huru hutumia kazi yake kujishusha kuwa chini yako ili huduma yake ikupe kumheshimu, Kumtambua na kumjali.  

Waafrika wenzangu; kama nafasi uliyonayo kwenye jamii ama shirika ama kampuni inakufanya kuwa COLONIAL MASTER wewe ni muathirika wa KIRUSI CHA UJINGA Kinachoitwa UTUMWA.
Ila uzuri ni kwamba kirusi hiki KINATIBIKA! Wahi Hosipitali ya Ufahamu.
Share on Google Plus

About The Light

0 comments:

Post a Comment